
Alhamdulillah ni siku nyingine tena na ninaimani sote tumeamka salama tumshukuru Allah Kwa zawadi hii ya uzima,awali ya yote napenda kukuuliza hivi Umewahi kujiuliza kwanini unaogopa sana kufanya kitu ulichopanga kukifanya kwa muda mrefu sasa ingawa unajua kabisa ni jambo jema kufanya na iwapo ukilifanya maisha yako yatavuka hatua nyingine muhimu na kuwa bora zaidi. Kila mara unapotaka kuanza kulifanya unajikuta unajiambia ni bora usubiri maana ukianza kulifanya hilo kwa muda huo lazima utashindwa. Matokeo yake ni kila siku umekuwa mtu wa kusitisha kufanya au unaanza unaishia katikati. Wakati mwingine umeanza kujilaumu na kujiona ni mtu ambaye huwezi kufanikiwa tena juu ya hilo.
Majibu ya sababu za hali hii yako mengi ila leo naomba nizungumze nawewe juu ya sababu moja inayochangia unashindwa kusogea mbele. Sababu hiyo ni kuwa uwezo wako wa kuvumilia mateso ya kukipata hicho kitu bado uko chini. Saikolojia ya mwanadamu inaweka wazi kuwa katika chochote unachotaka kukifanya sehemu ya ubongo wako inayohusika na matendo yasiyo ya hiari (unconscious mind) hupima kiwango cha mateso utakayo yapata kwa kufanya au kutokufanya hilo unalotaka kulifanya ikilinganisha na furaha utakayopata kwa kufanya au kutokufanya jambo hilo. Pale ambapo mateso yanapoonekana kuwa ni mengi kuliko furaha utakayopata unajikuta tayari umeamua kuahirisha kufanya ulichotaka kufanya pengine bila hata wewe mwenyewe kujiuliza.
Lakini pia saikolojia inaendelea kusema kuwa sehemu hii ya ubongo mara zote hutumia uzoefu wa taarifa za nyuma ulizowahi kuzipata ili kuchukua maamuzi wakati wa kupima kiwango cha furaha na mateso juu uamuzi unaouchukua. Hili linatupa nafasi ya kutambua kuwa kila mara tunapoanguka kuwa si kweli kuwa hatuna nguvu za kuendelea mbele na kufanya vizuri Zaidi bali ni kuwa hatuko tayari kuvumilia mateso tunayoyaona mbele tukilinganisha na furaha ya kuacha kufanya hilo.
Kitu kibaya ni kuwa maamuzi haya hufanyika bila ya sisi wenyewe kuhusishwa na baadae hupokea matokeo, lakini nafasi tuliyonayo ni kuuongeza uzoefu wetu juu ya uvumilivu wa mateso tunapoamua kufanya jambo ukilinganisha na furaha ya kitambo pale tutakapoamua kutokufanya. Ni lazima kama watu tuliodhamilia kushinda kuhakikisha nguvu yetu ya kuamini juu ya uvumilivu wa mateso ni kubwa kuliko upendo wa furaha ya kitambo, kila siku hakikisha unapata hamasa ya kukufanya kunasogea mbele mateso na kuvuka.
Mwandishi maarufu wa kimarekani Zig Ziglar aliwahi kusema “People often tell me that motivation doesn’t last. And I tell them that bathing doesn’t either. That’s why I recommend daily.” yaani “watu huniambia uhamasishaji hauishi, nami huwaambia ndivyo ilivyo kuoga pia. Hiyo ndio sababu ninasitiza iwe kila siku.” Alijua kama ulivyo mwili unawili na kupendeza huhitaji kusafishwa na maji safi kila siku ndivyo ilivyo pia nia (mind) ya mwanadamu inahitaji kulishwa mema kila siku ili iamue mema. Kuanzia leo jifunze kuushibisha ubongo wako maneno ya kutia moyo na kuamini ushindi unawezekana ili ushinde. Ukuze uwezo wako wa kuvumilia mateso utatoka ulipokwama.
Wewe ni mshindi,mwamshe shujaa ndani yako.
NAOMBA UTEMBELEE BLOG YANGU HII naythambis.blogspot.com UPATE KUJIFUNZA MAMBO MBALIMBALI PIA KWA USHAURI NAOMBA UNIANDIKIE UJUMBE KUPITIA +255689538628/nsalum998@gmail.com
#POSITIVETHOUGHT
#STRUGGLESREAL
#DREAMBIG

